Dakika chache zilizopita, Spika wa Bunge la Zimbabwe ametangaza kuwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe amejiuzulu na tayari ameshapokea barua yake . Kumekuwa na shangwe miongoni mwa Wabunge kufuatia tangazo hilo. harakati za kumuondoa madarakani rais huyo kupitia bunge zimesitishwa.Baada ya hatua hiyo, maelfu ya watu wamejimwaga barabarani kushangilia na kufurahia uamuzi hiyo.
Na Isri Mohamed/GPL






Post a Comment