Menu

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
 
Mbunge Nape Nnauye ametoa yake ya moyoni kwa kuhoji vyama vya siasa na wanasiasa Tanzania wanajifunza nini kufuatia mchakato wa uchaguzi ndani ya chama tawala cha (ANC) uliofanyika Afrika Kusini mwanzoni mwa wiki hii kumpata kiongozi wa chama hicho.

Chama tawala cha African National Congress (ANC) kilikuwa na uchaguzi wa ndani kumtafuta kiongozi wa juu ya chama hicho ambapo kulikuwa na zoezi la uchaguzi na nafasi hiyo kugombewa na wananchama wa chama hicho na kupigiwa kura, ambapo mwisho wa siku Cyril Ramaphosa aliibuka mshindi kwa kura nyingi zaidi dhidi ya Nkosazana Dlamini-Zuma hivyo Cyril Ramaphosa kutangazwa Rais wa (ANC). 
"Tunajifunza nini kwa mchakato uliopelekea kupatikana kwa Cryll Ramaphosa kama Mwenyekiti wa ANC!? Alihoji Nape Nnauye 
Uchaguzi wa Chama tawala nchini Afrika Kusini (ANC) ulitoa nafasi ya watu kugombea nafasi hiyo na kuleta ushindani ambapo wanachama wa chama hicho walipiga kura na kuweza kumpta mshindi ambaye ndiye alitangazwa kuwa kiongozi mku wa chama hicho. 

 

Post a Comment

 
Top