Menu

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Sarah wa Harmonize Ashindwa Kuvumilia Ampa Onyo Kali Wolper "Unamsumbua Mpenzi wangu Kwenye Simu "


Mpenzi wa msanii Harmonize, Sarah amemuonya ex-girlfriend wa muimbaiji huyo Jacqueline Wolper kwa kile alichodai muigizaji huyo anamsumbua sana mpenzi wake katika mitandao.

Aliweka wazi hilo ni Wolper ambaye ameweka wazi jumbe alizotumiwa na Sarah kupitia mtandao wa WhatsApp na kueleza kuwa hawezi kumjibu kwa sasa zaidi ya kumuhurumia.



Harmonize na Wolper walikuwa wapenzi kipindi cha nyuma na couple yao ilikuwa na nguvu sana yenye kukodolewa macho na vijana wengi. Walionekana kushibana katika mapenzi yao kiasi kwamba Harmonize aliweza hata kumshirikisha Wolper katika video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Niambie.

Baada ya kuachana Harmonize aliweka wazi kuwa katika mahusiano na Sarah binti kutoka nchini Italy na Wolper naye akawa na mahusiano na kijana maarufu mtandaoni, Brown, hata hivyo mahusiano yao pia hayakuchukua muda ukawa umevunjika.

Post a Comment

 
Top