Menu

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ akiwa na mpenzi wake.
MKONGWE wa Muziki wa Afro Pop Afrika Mashariki, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ anamaliza mwaka kwa kuachia video ya kibao chake kipya na cha kwanza kufanya na Taurus Musik, Baby.



Jide amesaini mkataba na lebo hiyo ya Kenya kwa miaka mitatu, ambayo ndani yake, atatengeneza albamu mbili, ikiwemo pia albamu yake ya kwanza ya video. Katika video yake mpya, mwanamuziki huyo amemshirikisha mpenzi wake, Spicy ambaye ni raia wa Nigeria. Hii ni video ya pili kucheza pamoja na Spicy ambaye pia ni mwanamuziki, ya kwanza ikiwa ile ya ngoma yao waliyofanya pamoja, Together Remix.

“Ni mkataba mzuri kwangu kwa sababu umezingatia masilahi ya pande zote mbili, ile lebo pia ni kubwa hapa Afrika Mashariki, wanafahamu nini cha kufanya ili msanii atimize malengo yao na yake pia, kwa hiyo ni suala la kujivunia,” anasema Jaydee katika mazungumzo kupitia mtandao wa WhatsApp. “Nimemshirikisha Spicy kwa sababu anafit kwenye nafasi ile, ni msanii lakini kumbuka pia ni mwenza wangu, nadhani nitafanya video nyingi pamoja naye, hata kumi ikibidi, kwani kuna ubaya wowote?”

Post a Comment

 
Top