Msanii
wa nyimbo za Injili nchini Tanzania Emmanuel Mbasha amefunguka na kuwatolea
uvivu mabinti wadogo na kusema saizi wengi wao hawaolewi kwa sababu wanawaza
starehe na hawafikirii kuhusu maisha zaidi ya starehe zisizo na tija.
Mbasha amesema kuwa kutokana na hali hiyo ndiyo maana vijana
wengi sasa wamekuwa wakioa wanawake wakubwa au ambao wamekomaa kiakili na
wanaowaza maisha na si starehe
"Vijana
wa sasa wamefocus na maisha zaidi, hivyo wanahitaji mwanamke aliyekomaa ubongo
ambaye wanaweza kufanya mipango ya maisha na kupaa kwa pamoja hadi kwenye ndoto
zao. Hii ndiyo inapelekea wanawake wenye umri mkubwa kuolewa kwa kasi kubwa.
Hivi vichenchede vinavyowazia kubandika kucha na kope bandia na kusingizia
mahusiano ya uongo ili kupata Kiki na mimba hewa sasa havina soko vimebakia
kuchuna viinua mgongo vya wanajeshi wastaafu" alisisitiza Mbasha







Post a Comment