Menu

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi amesema Tanzania inatarajia kupeleka wataalamu wake wa masuala ya intelijensia nchini Israel kwa ajili ya kupatiwa mafunzo maalumu.
Dkt. Mwimyi amezungumza hayo Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumpokea Waziri wa Ulinzi wa Taifa ka Israel Avigdor Liberman na kusema wamekubaliana kuhakikisha wanaimarisha mambo yakiusalama ndani na nje ya nchi hizi mbili na kubadilishana mbinu mpya za kupambana na wahalifu hata kwa zile njia ambazo ni ngumu kufikia katika hali ya kawaida.
"Mchango wa Israel katika teknolojia duniani ni mkubwa sana hivyo ni vyema nchi kuhakikisha wananufaika nayo katika nyanja zote hasa zile zinazotegemea Tehama kwani nchi hiyo ni moja ya nchi yenye tekinolojia ya hali ya juu sana duniani hasa kwa mambo ya kiusalama, ulinzi na mashine mbalimbali zikiwemo zile za matibabu", amesema Dkt. Mwinyi.
Kwa upande wake Waziri wa Ulinzi wa Taifa la Israel Avigdor Liberman amesema uhusiano wa nchi hizo mbili ni mkubwa na wamuda mrefu ndio maana wameamua kuleta tekinolojia za kiusalama ili kuilinda Tanzania na wahalifu sambamba na hapo wataendelea kutoa ushirikiano wao kwa ujuzi na ugunduzi wa tekinolojia mbalimbali hasa zinazohusiana na usalama wa nchi.


Post a Comment

 
Top