Aliyekuwa
Makamu wa Rais wa TFF Michael Richard Wambura ambaye jana amefungiwa maisha
kutojihusisha na masuala ya soka, amesema hukumu hiyo imetolewa bila yeye
kuhusishwa wakati alionana na Rais kabla ya maamuzi hayo.
Taarifa ya TFF iliyotolewa jana ilieleza kuwa Wambura alibainika
na makosa matatu ya kimaadili ikiwemo kugushi nyaraka za Shirikisho pamoja na
kupokea fedha kinyume na taratibu vitendo ambavyo vimetafsiriwa kuwa ni
kulishushia hadhi Shirikisho hilo.
Baada ya
maamuzi hayo Wambura amejitokeza na kuweka wazi kuwa katika huku hiyo
hajashirikishwa kwa lolote hata kuitwa kutoa utetezi wake licha ya kukutana na
Rais Wallace Karia pamoja na Katibu mkuu siku chache kabla ya kikao cha Kamati
ya nidhamu.
Aidha Wambura
ameenda mbali zaidi na kusema kuwa kweli amegushi nyaraka za TFF kwanini jeshi
la polisi halijahusishwa kwenye uchunguzi wakati ndio chombo chenye mamlaka ya
kuthibitisha hilo.
Wambura pia
amefafanua kuwa suala hilo limekuja baada ya yeye kuhoji juu ya uhalali wa
nafasi mbalimbali ndani ya shirikisho ikiwemo nafasi ya katibu mkuu ambaye
anatakiwa kuw awa kuajiriwa lakini kwasasa haiko hivyo.







Post a Comment