Menu

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Maua Sama Afunguka Kuhusu Kufunga Ndoa
MKALI mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Maua Sama kwa mara ya kwanza ametaja mwaka wa kuolewa kuwa mambo yakienda sawa mwaka huu unaweza kuwa wake.

Awali zilienea tetesi kuwa, staa huyo anayebamba na Ngoma ya Nakuelewa amechumbiwa na mpenzi wake ambaye ni Mzungu lakini mwenyewe ameibuka na kukanusha.

“Nilishangaa kwa kweli hilo suala la kuchumbiwa na Mzungu kwani halikuwa la kweli, kuhusu kuolewa nimekuwa nikisikia kwa mashabiki sana, ndoa ni mipango, maombi yao yanaweza kunifanya nikatimiza hilo na inawezekana hata mwaka usiishe,” alisema Maua.

Post a Comment

 
Top